promota mnaijeria aingia mitini ,dj apata kisago
heti vyombo vibovu ! haibu
Stuttgart,Ujerumani,
Usiku wa Jumamosi ya Tarehe 30.Augost 2014,
majira ya saa 10 alfajiri
Mwanamuziki nyota wa Bongo Flaver Nasib Abdul aka Diamond
Platnumz
alijukuta katika hali ya hatari hadi kuokolewa na Polisi mjini
Stuttgart,ujerumani,baada ya washabiki waliokuwa na hasira kuchoka kusubiri
show,washabiki hao waliokuwa wamelipa ticket euro 25 kwa kiingilio walihadiwa
kuwa show ingeanza saa 4.00 usiku,lakini walijukuta wakisubiri hadi majira ya
saa10 usiku au alfajiri ndipo mwanamuziki Diamond alipoletwa jukwaani na
promota wake raia wa
Nigeria anajiita kama Britts Event.
Hapo ndipo washabiki walipoona
kuwa hawakutendewa haki walianza kurusha chupa na kutaka kumvamia mwanamuziki
Diamond na promota wake,
Kilichowakera zaidi washabiki
ni pamoja na vyombo vibovu vilivyofungwa katika ukumbi huo kitu ambacho
kiliwafanya washabiki kuvunja hadi vyombo vya muziki
ma-Djs walishambuliwa na wapo
Hosptalini kwa sasa.moja wa Djs hao alipoteza Lap top yake ,mwanadada
DJ Flor alipatwa shock mstuko wa moyo na kukimbizwa hosptali,
washabiki hao walimpa kipigo DJ Drazee naye yupo hoi hospatal. Polisi
nchini ujerumani wanamesema tukio hili la haibu alijawahi kutokea,kuwa msanii kuchelewa
kufika jukwaani kwa ujerumani ni kitu cha hatari kwani washabiki wa ujerumani
wanaheshimu sana muda wao.
mpaka sasa polisi wanamsaka
mwandaaji wa onyesho hilo na wamesema kuwa
wanachunguza thamani ya hasara
hiliyosababishwa na ghasia hizo na pia itamfungulia mashataka promoter huyo
raia wa Nigeria,ambaye pia anachunguzwa kwa kusemekana anajihusisha na mtandao
fulani wa biashara.