TANGAZA NA TAZAMA HABARI

FANYA BIASHARA YAKO IJULIKANE ZAIDII jivunie kua mwanafamilia wa tazama habari ! WEAPON FOUNDATION TANGAZA BIASHARA YAKO NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI TUNAKUSHUKURU KWA KUA MWANAFAMILIA WA TAZAMA HABARI

Friday, September 5, 2014

MCHEKESHAJI NA MWANAMITINDO JOAN RIVERS AMEFARIKI JANA SEP 4 2014,

Tanzia: Mkosoaji maarufu wa mitindo ya mavazi 'Fashion Police', Joan Rivers amefariki September 4 akiwa na umri wa miaka 81. Binti yake Melissa amethibitisha kifo chake katika tamko alilolitoa kupitia US Weekly.
"Kwa masikitiko makubwa natangaza kifo cha mama yangu, Joan Rivers. Amepumzika kwa amani majira ya saa 7 na dakika 17 mchana akiwa amezungukwa na familia na marafiki wa karibu." Ameeleza Melissa katika sehemu ya tamko lake. Joan Rivers ambaye pia alikuwa comedian alizaliwa June 8,1933, Brooklyn, New York, Marekani. Na alianza kupata umaarufu miaka ya 1960 alipoanza kuonekana kwenye vipindi vingi vya TV. Apumzike kwa amani. Amina!