TANGAZA NA TAZAMA HABARI

FANYA BIASHARA YAKO IJULIKANE ZAIDII jivunie kua mwanafamilia wa tazama habari ! WEAPON FOUNDATION TANGAZA BIASHARA YAKO NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI TUNAKUSHUKURU KWA KUA MWANAFAMILIA WA TAZAMA HABARI

Thursday, August 7, 2014

Katiba ni ya watanzania sio ya wanasiasa wa Tanzania

Wabunge wa Bunge Maalum la Katiba wamegawanyika vipande viwili. Kipande kimoja kiko Dodoma kikiendelea na mchakato wa kujadili upatikanaji wa Katiba mpya.
Kipande kingine cha wajumbe wanaounda Bunge hilo maalum kimeendelea na na msimamo wake wa kugomea mjadala wa Bunge Maalumu la Katiba hadi watakapokubali kuheshimu maoni ya wananchi yaliyomo katika Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba.

Kipengele kinacholeta mzozo ni muundo wa serikali ambapo kundi linaloundwa na upande wa CCM linasimamia kwenye muundo wa muungano wa serikali mbili badala ya tatu zilizo katika rasimu hiyo.
Watu wa kada mbalimbali wakiwemo viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini wametoa ushauri wao kwa wajumbe wa Bunge hilo maalumu la Katiba wakiwataka kutumia busara zaidi badala ya nguvu katika kutekeleza jukumu hilo lililopo mbele yao.
Mbali na viongozi wa vyama vya siasa, wasomi, wanasiasa na wananchi wa kawaida vile vile wamekuwa na maoni, ushauri na maombi yao kwa wajumbe hao kurejea misimamo yao na kutazama mzigo waliopewa na wananchi
Wakati Bunge likiendelea watu wa kada mbalimbali, wasomi kwa wasiosoma, wafanyakazi, wafanyabiashara na wakulima, wote kwa ujumla wao neno lao ni moja kuwa watanzania wanataka Katiba itakayotokana na maoni na mapendekezo yao waliyoyatoa katika Tume ya warioba.
Ujumbe huo wa watanzania umeelekezwa moja kwa moja kwa makundi yote mawili yanayounda Bunge maalum, lile linalounda Ukawa na lile linalobebwa na Chama tawala CCM.
Watanzania walio wengi wanayatazama makundi yote mawili lile la Ukawa na lile la Tanzania kwanza (CCM) yanayounda Bunge maalumu la Katiba kama yenye ubinafsi na yaliyosahau jukumu walilopewa na wananchi, la kuwapatia Katiba mpya.
Kwamba makundi hayo yamewaweka kando wanaowawakilisha na kuamua kujiwakilisha wenyewe na vyama vyao. Kwamba mchakato unavyoonekana sasa ni kuwa umetekwa na wanasiasa kila kimoja kikilenga kujinufaisha.
Wachambuzi wa masuala ya siasa na Katiba wanasema kinachoonekana kukwamisha mchakato wa kupatikana kwa Katiba mpya ni ubinafsi wa wanasiasa na kwamba kinachopaswa kufanyika ni kwa wanasiasa wote waliopo ndani ya Bunge hilo maalumu kujivua uanasiasa wao na kubaki na Utanzania.
Kwamba wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba waweke pembeni upenzi, ushabiki na ukereketwa wa yale makundi yaliyowapeleka bungeni na kubakiza utanzania na uwakilishi wa wananchi.
Buberwa Kaiza, Mchambuzi wa masuala ya siasa na utawala bora nchini, anasema, wajumbe wa bunge maalumu wanapaswa watambue jambo moja kuwa wanawawakilisha wananchi na sio kujiwakilisha wenyewe au vyama vyao.
source mwananchi.