Kufuatia hofu ya
kuambukizwa ugonjwa huo hatari kwa kugusa au kuwa karibu na wagonjwa au miili
ya waliopoteza maisha kwa ugonjwa huo, ndugu wa marehemu wameripotiwa kuiburuza
miili ya ndugu zao kutoka majumbani kwao na kuitupa hovyo mitaani hali
inayoongeza hatari zaidi ya maambukizi.
Kwa mujibu wa Daily Mail, ugojwa huo hatari unaoweza
kusababisha mtu kutokwa na damu machoni, mdomoni na masikioni umeshaua
takribani watu 9,000 katika nchi za Afrika Mashariki.
Madaktari wanaohudumia
wagonjwa wa Ebola wanapata changamoto kubwa ya kukwepa maambukizi huku baadhi
yao wakiripotiwa kupata maambukizi na kupoteza maisha.
Hali ya hatari
imesababisha abiria wanaosafiri kutoka Afrika Magharibi kufanyiwa vipimo katika
viwanja vya ndege kwa hofu ya kuusambaza ugonjwa huo katika nchi wanazokwenda.