TANGAZA NA TAZAMA HABARI

FANYA BIASHARA YAKO IJULIKANE ZAIDII jivunie kua mwanafamilia wa tazama habari ! WEAPON FOUNDATION TANGAZA BIASHARA YAKO NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI TUNAKUSHUKURU KWA KUA MWANAFAMILIA WA TAZAMA HABARI

Friday, September 12, 2014

H Baba aeleza jinsi alivyotumia 150,000 tu kukamilisha video yake 'Tubabane', angalia na video yake hapa

Msanii wa miondoko ya Bongo Bolingo Flava, H Baba anaweza kuwa msanii wa kwanza mkubwa Tanzania kujitokeza hadharani kutaja kiwango kidogo zaidi alichotumia kushuti video ya wimbo wake.
Bila kung’ata neno wala kuongeza sifuri, H Baba akiwa kwenye kipindi cha
The Jump Off cha 100.5 Times Fm alieleza kuwa video ya wimbo wake mpya Tubebane aliofanya na muongozaji kutoka Mwanza ‘Saimaco’ ilimgarimu kiasi cha fedha za Kitanzania 150,000 tu.
“Unajua watu wengi wanaweza kukwambia ‘H Baba hatumuoni…’ waangalie video yangu niliyoshuti kwa 150,000 tu. Haina sifuri mbele. Ni laki na nusu na video inaitwa Tubebane. Ni bonge la video…”Alisema H Baba.
“Unajua sisi wasanii tusipende kuongea uongo kwa sababu uongo unaweza kutuletea matatizo. Matatizo ni yapi, mashabiki wanajua sisi tuna pesa kumbe pesa hatuna.”