TANGAZA NA TAZAMA HABARI

FANYA BIASHARA YAKO IJULIKANE ZAIDII jivunie kua mwanafamilia wa tazama habari ! WEAPON FOUNDATION TANGAZA BIASHARA YAKO NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI TUNAKUSHUKURU KWA KUA MWANAFAMILIA WA TAZAMA HABARI

Friday, September 12, 2014

MABASI YA UPENDO LA IRINGA NA SUPER FEO LA SONGEA YAGONGANA SABABU NI KUKWEPA PUNDA ALIYEKUA BARABARANI

 Basi la kampuni ya Super Feo likiwa limegongwa kwa nyuma na basi la Upendo leo asubuhi. 

Mabasi yote yanafanya safari kutoka Dodoma kwenda Iringa (upendo) na Super Feo (Songea) .

Taarifa za kutoka eneo la tukio zinasema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni punda aliyekatisha barabarani na  mwendo kasi wa basi la upendo bila umakini wa dereva wa basi hilo.


Abiria waliokuwa katika basi la upendo walisema kuwa  walikuwa wakilifuata basi la Super feo kwa kasi bila kuacha safety distance (nafasi ya usalama kati ya basi moja na lingine nyuma au mbele ) hali iliyopelekea ajali hiyo kutokea pale dereva wa basi la Super feo aliposimama ghafla kuepuka kugonga punda aliyekuwa akikatisha barabarani.

Taarifa zinaendelea kudai kuwa dereva wa basi la upendo amevunjika miguu na wengine wamejeruhiwa vibaya!