Boko Haram wazidi kumlaza macho Raisi Jonathan Moyo
Kundi la wapiganaji la kiislam la Boko
Haram,wamevamia shule moja ya mafunzo ya kipolisi.kituo hicho cha mafunzo
kilichoko kwenye kitongoji cha Gwoza kiko karibu na mpaka wa nchi ya Cameroon
ambacho hufundisha
maofisa wa Polisi nchini Nigeria.
Kikundi
hicha Boko Haram pia kinasemekana kuudhibiti mji wa jirani na Gwoza uitwao Buni
Yadi.
Nalo
shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch wametoa takwimu ya
vifo vilivyosababishwa na kundi hilo kua watu zaidi ya elfu kumi mpaka sasa
tangu walipoanzisha harakati za kutaka upande wa kaskazini mwa Nigeria uwe
chini ya utawala wa Kiislam.