TANGAZA NA TAZAMA HABARI

FANYA BIASHARA YAKO IJULIKANE ZAIDII jivunie kua mwanafamilia wa tazama habari ! WEAPON FOUNDATION TANGAZA BIASHARA YAKO NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI TUNAKUSHUKURU KWA KUA MWANAFAMILIA WA TAZAMA HABARI

Friday, August 8, 2014

KAMATI NO 2 YA BUNGE LA KATIBA YAKOSA THELUTHI MBILI KATIKA IBARA YA 19 NA 22


Dodoma. Kamati namba mbili ya Bunge Maalum la Katiba imekosa theluthi mbili katika ibara 19 na 22 zinaohusiana na maadili na miiko ya uongozi na utumishi wa umma.


Mwenyekiti wa kamati hiyo, Shamsi Vuai Nahodha alisema jana katika ibara ya 19 hawakupata theluthi mbili ya kura zilizopigwa kutoka Zanzibar.
Pia Nahodha alisema kamati yake ilikosa theluthi mbili ya kura zilizopigwa kwa upande wa Tanzania Bara katika ibara ya 22.
Alisema katika ibara ya 19 ambayo alikosekana mtu mmoja kutimiza theluthi mbili ya kura kwa upande wa Zanzibar.
Ibara hiyo inatamka kuwa kiongozi wa umma hatatumia ama kutumia au kuruhusu kutumika kwa mali za umma zikiwamo zilizokodishwa kwa Serikali kwa madhumuni ya kujipatia yeye binafsi ama kumpatia mtu mwingine manufaa yoyote.
“Kilichofanyika katika rasimu hii kulikuwa na neno kiongozi wa umma sasa wajumbe walio wengi wakafanya marekebisho kuwa si suala la kiongozi tu wa umma anayepaswa kuzingatia hili hata watumishi wa umma,” alisema.
Alisema kutokana na hoja hiyo wajumbe walio wengi wakaongeza neno mtumishi wa umma, jambo ambalo lilikataliwa na mjumbe mmoja kutoka Zanzibar ambaye alitaka ibara hiyo kusomeka kama ilivyo katika Rasimu ya Katiba.
Nahodha alisema kwa upande wa ibara ya 22, wajumbe walio wengi walitaka ibara hiyo ihamishiwe katika sura ya 11.
Ibara hiyo inahusiana na watumishi wa umma aliye katika ajira ya kudumu hataruhusiwa kuingia katika ajira nyingine ya kudumu yenye malipo ya mshahara.
Pia ibara hiyo inasema mtumishi wa umma atakayeamua kugombea, kuchaguliwa na kuteuliwa kushika nafasi ya madaraka ya kisiasa ya aina yoyote chini ya Katiba hiyo au uongozi wa ngazi yoyote katika chama cha siasa mtumishi huyo atachukuliwa kuwa utumishi wake umekoma tangu siku ya kuteuliwa kugombea, kuchaguliwa au kuteuliwa kushika nafasi ya madaraka ya kisiasa au uongozi katika chama cha siasa.
Nahodha , alisema mjumbe mmoja alipinga kuhamishwa kwa ibara hiyo katika sura ya 11 na kutaka ibakie katika sura hiyo.
Aidha, Nahodha alisema kulikuwa na mjadala wa kina kuhusiana na ibara zinazohusiana na rushwa.

 source mwananchi