TANGAZA NA TAZAMA HABARI

FANYA BIASHARA YAKO IJULIKANE ZAIDII jivunie kua mwanafamilia wa tazama habari ! WEAPON FOUNDATION TANGAZA BIASHARA YAKO NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI TUNAKUSHUKURU KWA KUA MWANAFAMILIA WA TAZAMA HABARI

Tuesday, September 2, 2014

DONDOSHA ‘MKONO WA SWETA’ NA IMANI POTOFU;

Wakati Serikali ikihimiza tohara ya mwanamume kama mbinu mojawapo mahususi ya kujikinga na maambukizi ya Ukimwi, bado zipo imani potofu zinazokinzana na juhudi hizo.

Matangazo ya redioni na kwenye mabango yanasema wazi kuwa mwanamume aliyetahiriwa anapunguza kwa asilimia 60 uwezekano wa kuambukizwa Virusi vya Ukimwi iwapo atafanya mapenzi na mwenzi mwenye virusi.
Kwa upande mwingine jamii ambako kampeni za tohara zinaendelea, kwa mfano jamii zilizoko mkoani Shinyanga zinao watu wanaoamini kuwa tohara ya mwanamume ni ‘suala la waswahili’. ‘Waswahili’ mkoani humo humaanisha waumini wa madhembu ya Kiislam.
Imani kama hizi haziji bila sababu. Ni kweli kwamba waumini wa dini ya Kiislam na wale wanaojiunga na madhehebu hayo, wanashauriwa kufanya tohara ya mwanamume kama mojawapo ya sharti muhimu.
Ukweli ni kuwa tohara ni jambo jema, liwe kwa ajili ya sababu za kiimani ama za kiafya tu. Hata vitabu vya kikristo, hasa Biblia Takatifu, inashauri wanaume kutahiriwa siku ya nane tu tangu kuzaliwa.
Wapo pia wanaoamini kuwa wanaume wenye umri mkubwa hawafai kufanyiwa tohara.
“Kweli kabla ya kuja kwenye sehemu ya tohara nilifikiri sana kwamba inawezekanaje kupona kidonda mimi mtu mzima hivi?” anahoji Denis Mabala, mkazi wa Nyankende, Kahama.
Wasiwasi wake ulimfanya awatangulize kwanza watoto wake ili kuona iwapo kweli vidonda vinavyotokana na operesheni ya tohara vinapona haraka.
“Baadaye nilifahamu kuwa walikuwapo hata walionizidi umri ambao walitahiriwa hivi karibuni na baada ya siku chache walirudia kufanya kazi zao, basi ndiyo nikaamua na mimi kwenda kutahiriwa,” anaongeza Mabala, huku akitabasamu.
Takwimu Wilaya ya Kahama
Kwa mujibu wa meneja wa huduma ya tohara ya mwanamume wa Hospitali ya Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Masaga Odhiambo, takwimu zinaonyesha wazi kuwa miongoni mwa wanaume wa rika lengwa (miaka 10-49) ni wale wa umri wa chini ndiyo hujitokeza zaidi.
Anasema wanaume wenye umri wa miaka 15-24, 652 wamejitokeza kufanyiwa tohara katika Kituo cha Hospitali ya Kahama, wakati wale wa umri wa miaka 25-34 wamejitokeza 113 tu tangu Januari mwaka huu.